Professor Jay ft Chameleone – Kwa Ajili Yako 
Sikiliza hii ngoma hapa:
New and old audio music will be posted here.
“Big 4 the Geez” ukipenda Unaweza Kumuita “Mwanamadharau” ama wengi walimuita “Geez Mabovu Jina kamili “Ahmed Ally Utepe” alikuwa ni Msanii wa Kizazi kipya aliyefanya mziki wa hip hop toka “Dirty South” Iringa, Tanzania. Geez alifariki dunia siku ya Tarehe 12 Mwezi wa 11 Mwaka huu baada ya kuumwa kwa muda mrefu. Wakati wa uhai wake alikuwa ni kati ya wasanii wachache ambao waliitendea haki Hip hop nchini Tanzania.
Haukujalisha Mziki huu ulimlipa kiasi gani katika soko la Muziki wa kizazi kipya nje na ndani ya Bongo, Mchizi aligangamaa na kuendelea kufanya kazi yake ya Sanaa tokana na Mapenzi ya sanaa na kazi yake. Mtoto huyu wa kiume hakuyumbishwa tokana na air-time rediaoni ama kuandikwa mara kwa mara katika blogs ama kutangazwa na vyombo vya habari kwa nia ya kumpatia kipato zaidi, alipiga moyo konde ingawa ilikuwa ni ngumu ila hakufa moyo. Alikuwa na Urafiki wa karibu na wasanii toka Chemba Squad pia wasanii kadhaa toka Arachuga A-town city.
Mimi pia nilikuwa ni shabiki mkubwa wa kazi zake na nilivutiwa zaidi na Style yake ya Kughani pamoja na sauti yake nzito ukilinganisha na umbo lake, pia mashairi yake ambayo yalikuwa ni ya kitaa zaidi yalikuwa yamesheheni aliweza ujumbe ulioeleweka kirahisi pindi ukimtegea sikio. Siku 3 baada ya Kifo chake nilipokea Maombi mengi toka kwa washabiki wake wakiniomba nifanye (Non-Stop) Mix ambayo itaenzi mziki wa GEEZ MABOVU nami sikufanya ajizi. Basi kama wewe ni Mshabiki wake wa kweli na ungependa kuendelea kumkumbuka Fanya kubofya link hii hapa chini usikilize/uipakue Mix hii Bure kama kumbukumbu ya kazi za Geez. #ForTheLoveOfHiphop #GeezMabovuTributeMix #RIPDirtySouthDawg

Mashabiki wote wa Bongo Hip hop, hii ni zawadi mpya toka kwa The GENERAL himself, toka katika Kundi la watengwa. This time amekuja na GHETTO LOVE joint, ambayo itakufanya moyo wako ukusisimuke. JCB ameachia “Mtoto Mkali” leo Rasmi kwa wana wote na wapenzi wa Hip hop baada ya muda kidogo maana yupo mbio na shughuli zake za maisha. Ngoma ni kali, Support Bongo Hip hop kama wewe ni mpenzi wa kweli wa huu mziki. Click link hii kuweza kuusikiliza na kuupakua hapa chini:
Download MP3:


Hii hapa ngoma mpya ya YOUNG KILLER akimshirikisha kaka yako toka Rock City Mwanza FID Q. Ngoma hii ina michano ya kweli sana. Kama wewe ni mpenzi wa Bongo Hiphop na unafuatilia kazi za hawa jamaa, fanya kuingia YouTube hapa chini ku-enjoy hili dongo. Naambatanisha mashairi ya huu wimbo baada ya video, Enjoy!
Stream the audio here:
VERSE 1:
Mama ndie alie nitabiri mi nitakua star na nyota wa kila pande/
Nikiwa na raha.. kwa mwenye hasira nisijigambe/
Usimpige mkeo piga shangwe/
Kwa maana Young killer sio ngazi.. kwa hiyo mwambieni shetani asinipande/
I Think big.. its my dream biggie kuwa/
Bigger wa michano nigga ambaye hata Jigga atanijua/
Kuwa msodoki nawaficha mistari/Upeo wangu umekula mchicha na ndo maana nina fikra za kuona mbali/
Msukuma anae sukuma mitikasi ikatulia/
Hata ‘ Francis Cheka ‘ naweza mpiga panchi akalia/
Wanaoijua njaa ndo wanaamini cha kwanza kilimo/
Mi sijagombania ustar ili nikifa nikazikwe kino/
Wabovu wakichana ‘ IMO ‘ na hawazijui nguzo tano/
Leo kwenye ustar ‘ simo ‘ kisa sina muonekano?/
Mi nina POWER.. ya ibada nilioiomba baada ya kipato/
Pole dada ulie nitosa kisa umenizidi kidato/
Futa jasho na damu saka noti ‘hali tete’ /
Watoto wanamjua Diamond na Joti”” zaidi ya Kikwete/
Popote niko fiti…tega skio/
Shoga hata akitoa jicho vipi…hawezi kuyaona mafanikio..ndio
Chorus:
Ni MSODOKI na NGOSHA.. Miujiza iliyotabiriwa haina haja ya kuogopa/
Nafasi nilizozichezea yawezekana zisirudi/Lakini ninaweza zitengeneza nikiongeza juhudi/
Tangu Agosti tangu April.. YEAAAH.. tangu Agosti tangu April/
Nina Hustle bila wasi wala hofu/ MUNGU wangu hawezi nipa shida ambayo nitashindwa kuisolve
VERSE 2:
Wakisha amini unawahitaji zaidi ya wanavyokuhitaji/
Mapenzi ya ‘ wadau wa mjini ‘ hugeuka ya ‘ samaki na maji ‘/
Uishi ndani yake tu… nje yake uvuliwe/
Kwa msaada wake upikwe kisha yawanawishe.. uliwe/
SIKUUMBWA nije kusettle for less/
Nitaisubiri mvua inyeshe.. nijitokeze kudance/
Nonsense sitemi/ asset sio deni/ HOMEBOY.. natema vitu on point.. jifunzeni/
THAMINI HUU MUDA kabla haujageuka HISTORY/
Part of the PAST dont fit the script for the FUTURE memory/
Niliyoyapitia… yameniandaa kwa haya yajayo/
Sio dalili ya kusinzia.. ni ‘ NJAA ‘ nikipiga mihayo/
MASKINI.. ninajiamini hadi natokwa na ukungu/
Bila ujuzi wasingenithamini.. NINGETOSWA mpaka na ndugu/
Kitachonizamisha sio kudondoka mtoni/
Ni kushindwa kupiga mbizi na kusizi ili msinione…
Ni MSODOKI na NGOSHA.. Miujiza iliyotabiriwa haina haja ya kuogopa/
Nafasi nilizozichezea yawezekana zisirudi/Lakini ninaweza zitengeneza nikiongeza juhudi/
Tangu Agosti tangu April.. YEAAAH.. tangu Agosti tangu April/
Nina Hustle bila wasi wala hofu/ MUNGU wangu hawezi nipa shida ambayo nitashindwa kuisolve
VERSE 3:
FQ-
Napenda umaarufu.. ninachukia MBWEMBWE zake/
Au ninapospit truth kwa booth halafu WAKUSHI hamninyaki/
Ninauacha uchi ‘ UKWELI ‘ uzushi sio mwake/
Hata mkigushi mtafeli.. hamnigusi na hamnipati/
YK-
Siamini nimekua MIMI hadi hii leo nimefika hapa/
Aliyenilea hakuniamini.. niliyemtegemea hakunitaka/
Bila nyinyi.. WADAU.. Ninakili sishiki sarafu/
Na ndo maana sili bata kwa maana BATA WACHAFU/
Kuwa mkali wa kusifiwa.. kubali kutumiwa/
Nilichoambiwa kuwa ‘ sikuhizi hadi wajanja wanaliwa’/
Inatakiwa kuwa STRIKER..Mambo yaende SCHKOPA/
Kama haujanileta.. hauwezi kunirudisha nilikotoka…
Download MP3:

Kwa wale watu wangu tunao support Mziki wa Bongo hasa Bongo Hip hop Check out New Banger toka Kwa MWANAHAPA. Ngoma hii ambayo ni ya Ukweli ina ujumbe mzito katika jamii yetu inaitwa BWANA MDOGO Chini ya Uangalizi wa PRODUCER: SALLII TEKNIKS na Kufanyiwa MIXING na JAY ADEAN Katika Studios za ROCK TOWN RECORD.
Bofya hii link hapa chini Uisikie/Uipakue. Enjoy!

Stream this Audio here:
Download MP3:


Bongo Hip hop Mix June 2014 ©️ DJ NGOMANAGWA
For individuals who have a deep appreciation for quality hip hop music, particularly the boom bap style, you have arrived at the perfect destination. The mix titled “Bongo Hip Hop Mix June 2014,” curated by DJ Ngomanagwa, was uploaded a decade ago. I have chosen to re-upload it due to the previous link becoming inactive. Immerse yourself in the vibrant sounds of Tanzanian hip hop and please remember to share your thoughts in the comments section.
Bongo Radio Throwback Monday Show June 2nd 2014 Part 1(C)Ngomanagwa.
Hii ni Show ya Jana yenye Ngoma za Zamani za Afrika Mashariki. Hili ni Saa la Kwanza la Show na Lisaa la Pili nitali-upload Alhamisi hii. Enjoy Good Music and Show, Stay Blessed.
Oldskool Bongo Finest May 2014 (C)Ngomanagwa.
Hii Hapa ni Mix Fupi yenye ngoma chache ambazo ziliwahi kuvuma na moja mbili adimu. Kwenye hii Mix utasikia wasanii na makundi kama Hard blasters, Kwanza Unit, Deplowmatz, Suma G na Hashim Dogo. Ukipenda Unaweza kuisikiliza na Kuishusha HAPA>>>http://hu.lk/guz6bejj01z4