
Tokana na Malalamiko toka kwa wasikilizaji wa Mixes na Wapenzi wa Mziki wa Bongo kuwa nabagua kufanya Mixes za Miziki mingine na Kufanya Bongo Hip hop Mixes peke yake ama Sana. Nimesikia Kilio chenu na Nawaletea NEW Mix ya “BONGO FLAVA” kwa Mwezi “MAY” Mwaka 2014 kwa ajili yenu. Nyimbo zote humu ni Mpya. Enjoy
Category: AUDIO
New and old audio music will be posted here.
Bongo Radio Throwback Monday Show May 12th 2014 (C)Ngomanagwa
Bongo Radio Throwback Monday Show May 12th 2014 (C)Ngomanagwa.

Kama Ungependa kuisikiliza ama Kuidownload Show Ingia hapa>>>http://hu.lk/7yn80h1fk2kg
(Audio) Big Dogg Posse “BDP Kamili”

Hawa ni Vijana Kutoka Kinondoni wanaokwenda kwa Jina la Big Dogg Posse. Kundi hili liliundwa Mwaka 1994 na lilikuwa na Jumla wa wasanii watatu waliokuwa wakiwakilisha. Majina ya wasanii hao ni KOMPYUTAH, DRAYZI CHIEF and CHRONIC FINGER. Mwaka 2000 walitoka na Single yao matata ambayo ilikuwa ni Bonge la Hit katika maredio na Matamasha iliyokwenda kwa jina la “Rudi Mpenzi” waliyoifanya katika Studio za MJ pale Oysterbay. Pia walitoa Ngoma nyingine kama “Wosia” pamoja na “Bahati ya Mwenzio” ambazo zilikuwemo katika album yao ya Kwanza.
Kutokana na Kufanya Vizuri katika Soko la Muziki wa Kizazi Kipya Vijana hawa wa Kinondoni Waliingia Studio Kufanya Santuri ya Pili iliyokwenda kwa Jina la “BDP KAMILI”. Santuri hii ilibeba Ngoma kama “Ma jobless” ambayo ndio ilikuwa Single yao ya kwanza ambayo ilifuatiwa na “Kumwambia” na nyinginezo kibwena. Kwa Kifupi walitikisa sana Jiji la Dar na Vitongoji vyake mara walipopanda kwenye Majukwaaa ya Matamasha na Walikuwa na wapenzi wengi sana. Mziki wao ulikubalika sana ndani ya Bongo. Bofya hapa Kusikiliza Ngoma zao Mbili toka katika Santuri yao ya Kwanza.

(Audio) New Bongo Hip hop Mix April 2014 (C)Ngomanagwa
Karibuni wale wote wenye Kiu ya Mawe mapya ya Bongo Hip hop ambayo yamo katika hii Non-Stop Mix yenye Ndonga za Ukweli zilizotoka hivi karibu pamoja na moja mbili zilizotoka … Continue reading (Audio) New Bongo Hip hop Mix April 2014 (C)Ngomanagwa
(Audio) Tha De-Plow-Ma-TZ

De-Plow-Matz
Members: Dola, Saigon, Stigo, Trip Dogg
Albums: Are you down with the DPT (96), Tha De-Plow-MaTZ (97)
Katikati ya Miaka ya 90’s, Saigon na Stigo waliungana na Dola Soul ambaye alikuwa ndio amerudi toka Lagos nchini Nigeria alipokulia. Walianza Kurekodi Ngoma chache katika Studio na P- Funk na Master Jay na Matokeo yake ilikuwa ni Santuri ya De-Plow-Matz. Style zao za Ku-Flow zilikuwa ni mpya katika masikio wa wapenzi wa Mziki wa kizazi kipya nchini Tanzania. Ngoma walizowahi Kuzitoa kama Kundi ni kama, ” Turuke kwa Furaha, Are You down, Tanzania” pia Solo Track ya Saigon iliyoitwa, ” Take a ride” ambazo zilikuwa maarufu sana katika vituo vya Redio na TV.
Mnamo Mwaka 1999 Members wote wa De-Plow-Matz walikuwa wameondoka Bongo Kuelekea Ughaibuni kwa Masomo akiwemo Saigon, Trip Dogg pamoja na Stigo na Kumuacha Dola Soul Peke Yake akiendelea Kuipeperusha Bendera Ya Kundi. Hapo Jamaa akaamua kufanya Solo Album ambayo ilipata Mafanikio Sana ndani ya Bongo ambayo ilikuwa na Ngoma Kama, “Nani na nani, Kwenye Chati n.k” Sasa Hivi Dola Yupo Chicago akiishi na Familia yake, Saigon alirudi Bongo na anaendelea kufanya mziki, Stiggo Yupo New York akiishi pamoja na Ku Produce Mziki katika Studio za S&S na Trip dogg yupo UK. Kwa Historia hii fupi ya kundi hili, Sikiliza Ngoma zao tatu hapa ikiwemo Track Moja ambayo Dola Alifanya kama Solo Artist. Bofya hizi Links kuweza kusikiliza hizi Nyimbo.






